Aidha, Mwanasheria MKuu wa Mahakama ya Wilaya Bw.James Emmanuel Mhoni amefafanua kuwa wiki ya Sheria ni kiashiria Cha kuanza kwa shughuli za sheria hivyo sheria inatoa fursa kwa Wananchi kujifunza umuhimu wa sheria na kutambua majukumu ya Mahakama jinsi inavyotumia sheria hizo kutekeleza majukumu ya kazi zake na zinavyomsaidia mwananchi katika kutafuta Haki na kupata Elimu kuhusu sheria hii itawafungulia njia ya kujiamini na kufika mahakamani kuwasilisha kesi zenu zote zitasikilizwa.
Maadhimisho hayo ya Wiki ya sheria yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Kisiasa, Katibu Tawala Wilaya,Mkurugenzi Mtendaji , Jeshi la Wananchi, Jeshi la kujenga Taifa, Jeshi la Akiba, Viongozi wa Dini mbalimbali Wanafunzi na Wananchi wa kutoka vijiji na Kata mbalimbali Kuungana Kuadhimisha.


Copyright ©2021 Wanging'ombedc . All rights reserved.